Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kuboreshwa kwa teknolojia kunaweza kuokoa maisha kupotea majanga kwa mujibu wa ripoti wa shirika mwezi mwekundu

Kuboreshwa kwa teknolojia kunaweza kuokoa maisha kupotea majanga kwa mujibu wa ripoti wa shirika mwezi mwekundu

Kutokuwepo uwezo wa kupata habari na ukosefu wa teknolojia kumekuwa na athari kubwa kwa uwezo wa watu kujiandaa na kurejea hali yao ya kawaida baada ya kutokea kwa majanga kwa mujibu wa ripoti kuhusu majanga ya mwaka 2013 iliyotolewa na shirika la kimataifa la msalaba mwekundu na lile na mwezi mwekundu. Ripoti ya mwaka huu inaangazia zaidi teknolojia. Ripoti hii imeandikwa na wataalamu wa masuala ya kibinadamu 40 na wasomi na inaeleza kuwa baada ya masaa machache baada ya kutokea kwa janga maisha yanayookowa uokolewa na watu wa kawaida wengi wakiwa hawana ulewa wowote wala vyombo vya mawasiliono. Hata kama idadi ya watu waliaoothiriwa na majanga ilipungua mwaka 2012 idadi ya watu walioathiriwa kwenye nchi maskini iliongezeka ambapo watu zaidi ya milioni 31.7 waliathiriwa.