IOM imepokea dola milioni 2 kuwasaidia Wahaiti walio makambini, yakarabati nyumba za waliopoteza makazi Syria.
Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM limesema limepokea dola milioni mbili kutoka serikali ya Sweden kama mchango wa kuwalinda wananchi zaidi ya laki mbili walioathirika kufuatia tetemeko la ardhi mwezi Januari mwaka 2010 nchini Haiti
Msemaji wa IOM Jumbe Omari Jumbe anafafanua namna msaada huo utakavyotumika
(Sauti ya Jumbe)
Wakati huo huo shirika hilo la kimataifa la uhamiaji IOM linakarabati nyumba za raia waSyria waliokosa makazi kufuatia mgogoro unaoendelea ambako huko Damascus nyumba 41 zimekarabatiwa kwa kipindi cha miezi mitatu. Akizungumzia hilo Jumbe Omari Jumbe anasema
(Sauti Jumbe)