Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Sehemu za ibada zatumika kutoa tiba Uganda: UNICEF

Sehemu za ibada zatumika kutoa tiba Uganda: UNICEF

Huduma ya afya ya msingi ni jambo muhimu kwa jamii ili waweze kushiriki shughuli za maendeleo. Hata hivyo katika maeneo mengi ya nchi zinazoendelea Uganda ikiwa ni mojawapo, watu hulazimika kwenda mwendo mrefu kupata huduma hizo na hivyo kusababisha kukosa huduma au kuipata wakati wameshachelewa. Kwa mantiki hiyo Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, limebuka na mpango mpya nchini Uganda. Je ni upi huo? Ungana na Joseph Msami katika ripoti hii.