Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kuendeleza mazingira safi hakupotezi nafasi za ajira: ILO

Kuendeleza mazingira safi hakupotezi nafasi za ajira: ILO

Mratibu wa progamu ya ajira ya shirika la kazi duniani ILO Peter Poschen ameonya juu ya uwezekano wan chi zilizoendelea kukubwa na tatizo la tabia nchi kama zitaendelea kupuuza kuchukua hatua kuunga mkono kampeni ya inayohimiza uchumi unaojali mazingira.

Mtaalamu huyo amesema iwapo dunia itazingatia na kuweka sera sahihi na kuzitekeleza kwa vitendo, kunaweza kushuhudia kupatikana kile alichokiita faida mara mbili, ile ya kimazingira nay a kijamii. Amesema kuwa hatua hiyo pia inaweza kutoa msukumo wa kimaendeleo na kuongeza nafasi za ajira kutoka milioni 15 hadi 60 katika kipindi cha miongo miwili ijayo.

Amezungumzia pia uwezekano wa kuwakwamua zaidi ya wafanyakazi milioni 10 walioko kwenye lindi la umaskini.Hata hivyo,  anasema hili halitakuwa rais. Kwa nini?