Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkutano wa upokanyaji silaha umesikia mapendekezo ya kumaliza mvutano

Mkutano wa upokanyaji silaha umesikia mapendekezo ya kumaliza mvutano

Mkutano kuhusu upokonyaji silaha unaofanyika mjini Geneva Jumanne umesikia mapendekezo ya mataifa 13 yanayoeleza jinsi gani ya kumaliza vikwazo vinaoukabili mkutano huo.

Balozi Luis Galeeogos Chiriboga wa Equador ambaye ni Rais wa mkutano huo amesema mkutano unahitaji kuwa na mjadala wa wazi ili kufungua njia na kupata matunda wanayotarajia.

Wajumbe katika mkutano huo wameelezea kuchanganyikiwa kwao kutokana na mvutano wa miaka 15 unaosababisha mkutano huo kutopiga hatua. Jason Nyakundi anaripoti

(RIPOTI YA JASON NYAKUNDI)