'Wahamiaji waliorejea Sudan kusini wakabiliwa na matatizo magumu makwao': IMO
Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM), ambalo ni miongoni mwa jumuiya za kimataifa zinazoshirikiana kikazi kwa ukaribu zaidi na UM, limewasilisha ripoti mpya iliotolewa Geneva hii leo, inayozingatia hali ya wahamiaji wa ndani ya nchi pamoja na wahamaji wazalendo waliorejea Sudan Kusini kutoka mataifa jirani na kutoka nje.