Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR kuhamisha tena wahamiaji wa Dadaab, Kenya

UNHCR kuhamisha tena wahamiaji wa Dadaab, Kenya

Andrej Mahecic, msemaji wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) aliripoti leo kutoka Geneva kwamba taasisi yao imeanzisha rasmi, wiki hii, operesheni za kuwahamisha wahamiaji wa Usomali 12,900 kutoka kambi ya Dadaab, iliosongamana watu kupita kiasi, na kuwapeleka wahamiaji kwenye kambi ya makaazi ya muda ya Kakuma, iliopo kaskazini-magharibi nchini Kenya.