Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kusambaa kwa madawa ya kulevya Guinea kunautia wasiwasi UM

Kusambaa kwa madawa ya kulevya Guinea kunautia wasiwasi UM

Shirika la Polisi wa Kimataifa juu ya Makosa ya Jinai (Interpol) pamoja na Idara ya UM juu ya Udhibiti wa Madawa ya Kulevya na Uhalifu (UNODC) baada ya kufanya ziara ya uchunguzi katika taifa la Guinea, kwa ushirikiano wa karibu na Mjumbe Maalumu wa KM kwa Afrika Magharibi, ilifichua shughuli haramu za kuzalisha, kimagendo, madawa ya kulevya huendelezwa nchini humo.