Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM apongeza kuachiwa huru kwa wanahabari wa Marekani katika DPRK

KM apongeza kuachiwa huru kwa wanahabari wa Marekani katika DPRK

Taarifa ya Ofisi ya Msemaji wa KM iliotolewa Ijumatano asubuhi imesema Bani Ki-moon ameukaribisha, kwa ridhaa, uamuzi wa Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Umma wa Korea (DPRK) wa kuwaachia huru waandishi habari wawili wa Kimarekani, kwa sababu za kiutu, wanahabari ambao walikabidhiwa Raisi mstaafu wa Marekani Bill Clinton jana Ijumanne, alipokuwa anazuru mji mkuu wa Pyongyang.