Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mapigano ya karibuni Mogadisho yawaong'olesha makazi 200,000 ziada, imeripoti UNHCR

Mapigano ya karibuni Mogadisho yawaong'olesha makazi 200,000 ziada, imeripoti UNHCR

Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limeripoti, kwa kupitia msemaji wake aliopo Geneva, kwamba muongezeko wa mapigano yaliovuma karibuni kwenye mji wa Usomali, wa Mogadishu, ni hali iliozusha athari mbaya kabisa kwa wakazi waliolazimika kuhama mastakimu yao, na kuleta usumbufu mkubwa kwa raia wa kawaida.