Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mawasiliano ya simu za mikononi yatazamiwa kuhamasisha mapinduzi kwwenye utabiri wa hali ya hewa Afrika

Mawasiliano ya simu za mikononi yatazamiwa kuhamasisha mapinduzi kwwenye utabiri wa hali ya hewa Afrika

Baraza juu ya Misaada ya Kiutu Duniani, na Raisi wake, KM wa UM mstaafu Kofi Annan, akijumuika na kampuni ya mawasiliano ya Ericsson, Shirika la UM juu ya Utabiri wa Hali ya Hewa Duniani (WMO), na vile vile kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi, Zain, pamoja na Taasisi ya Huduma za Maendeleo Duniani ya Chuo Kikuu cha Columbia, Marekani wote pamoja wametangaza, leo hii, taarifa ya kufadhilia mradi mkuu, unaojulikana kama "Mradi wa Taarifa za Hali ya Hewa kwa Wote", ambao ukitekelezwa una matumaini ya kuwasilisha mapinduzi ya kuridhisha katika kuimarisha zaidi uwezo wa kusimamia mtandao wa utabiri wa hali ya hewa, hususan kwenye yale mazingira yanayoendelea kuathiri hali ya hewa barani Afrika.