UNEP kuanzisha mradi mpya kuhishimu wajasiri wa kudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa
Shirika la UM juu ya Hifadhi ya Mazingira (UNEP) limeanzisha mradi maalumu wa kuihishimu ‘Siku ya Mazingira Duniani’ utakaowatambua wale watu wanaoshiriki kwenye juhudi mbalimbali za uvumbuzi mpya na usio wa kawaida wa kuamsha hisia za umma kutunza mazingira.