Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR na Wakf wa Mandela waazimu kupiga vita bia chuki za wageni Afrika Kusini

UNHCR na Wakf wa Mandela waazimu kupiga vita bia chuki za wageni Afrika Kusini

Shirika la UM Linalohudumia Wahamiaji (UNHCR) pamoja na Taasisi ya Wakf wa Nelson Mandela (NMF) wamejumuika kwenye kadhia muhimu ya kupiga vita lile janga la hatari kuu inayochochea chuki za wazalendo dhidi ya wageni katika Afrika Kusini, tatizo ambalo mwaka jana lilisababisha mauaji ya wageni 62, wingi wao wakiwa wahamiaji kutoka nchi za Afrika pamoja na watu wenye kuomba hifadhi ya kisiasa.