Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

IFAD inasisitiza ruzuku kwa wakulima masikini ndio ufunguo wa kuuvua ulimwengu na mzoroto wa uchumi

IFAD inasisitiza ruzuku kwa wakulima masikini ndio ufunguo wa kuuvua ulimwengu na mzoroto wa uchumi

Kanayo Nwanzeon, Raisi wa Shirika la UM juu ya Mfuko wa Kimataifa kwa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) ameyasihi mataifa yenye maendeleo ya viwanda kuharakisha misaada yao maridhawa kwa wakulima wadogo wadogo, hasa wale waliopo katika nchi masikini, ruzuku ambayo anaamini ikitekelezwa kidharura itasaidia sana kwenye zile juhudi za kuuvua ulimwengu na mzoroto wa uchumi uliotanda kimataifa sasa hivi.