Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tume ya UM yatoa mwito kuimarisha juhudi za huduma Zimbabwe

Tume ya UM yatoa mwito kuimarisha juhudi za huduma Zimbabwe

Tume maalum ya idara za UM huko Zimbabwe imesisitiza kwamba hali ya kibinadamu inaendelea kua mbaya sana na kuhimiza serekali na jumuia ya kimatiafa kusaidia kuimarisha juhudi za msaada wa dharura.

Tume hiyo iliyo ongozwa na naibu mratibu wa Idara ya Huduma za Dharura za UM Bi Catherine Bragg wiki hii ili tathmini kiwango cha msaada unaopelekwa miongoni mwa mambo mengine, ili kuweza kukabiliana na mzozo wa chakula unaowakumba watu milioni 7.