17 Novemba 2008
Mwigizaji wa kike wa michezo ya sinema kutoka Afrika Kusini na Marekani, Charlize Theron leo ameidhinishwa rasmi na kukabidhiwa wadhifa wa Mjumbe Maalumu wa UM kwa Amani, na anatumainiwa kuchangisha huduma zake kwenye juhudi za kukomesha udhalilishaji na utumiaji mabavu dhidi ya wanawake, hususan katika bara la Afrika.~