Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uholanzi imebuni maabara maalumu itembeayo kuisaidia UNEP kukabili maafa

Uholanzi imebuni maabara maalumu itembeayo kuisaidia UNEP kukabili maafa

Serikali ya Uholanzi imewasilisha aina ya maabara maalumu ya magari iliobuniwa kutumiwa kukabiliana na dharura za kimazingira kimataifa. Mabara ya aina hii itatumiwa kulisaidia Shirika la UM juu ya Hifadhi ya Mazingira (UNEP) kupata uwezo wa kusafiri, kwa haraka, kwenye maafa ya dharura ya kimazingira ili kupima, kwa utaalamu unaoaminika, hali kwa kuhusiana na vitu vya sumu vinavyohatarisha maisha. Maabara hii itajulikana kama Maabara ya Kutathminia Hali ya Mazingira (EAM) na itakuwa inapelekwa kwenye mataifa yanayoendelea yaliokosa utaalamu na uwezo unaohitajika kudhibiti kidharura maafa ya kimazingira.~