Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UN-HABITAT imetia sahihi makubaliano ya UM kushiriki kwenye Maonyesho ya Dunia ya Shanghai 2010

UN-HABITAT imetia sahihi makubaliano ya UM kushiriki kwenye Maonyesho ya Dunia ya Shanghai 2010

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Makazi (UN-HABITAT) yaani Anna Tibaijuka mapema wiki hii ametia sahihi maafikiano maalumu nchini Uchina yatakayoiwezesha UM na mashirika yake kadha kushiriki kwenye Maonyesho Makuu ya Dunia ya Shanghai katika 2010, maonyesho ambayo yatalenga zaidi nidhamu mpya za kuimarisha miji na maendeleo.