21 Agosti 2008
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Makazi (UN-HABITAT) yaani Anna Tibaijuka mapema wiki hii ametia sahihi maafikiano maalumu nchini Uchina yatakayoiwezesha UM na mashirika yake kadha kushiriki kwenye Maonyesho Makuu ya Dunia ya Shanghai katika 2010, maonyesho ambayo yatalenga zaidi nidhamu mpya za kuimarisha miji na maendeleo.