Baraza la Haki za Binadamu linazingatia haki za wanawake
Louise Arbour, Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu aliwaambia wajumbe waliohudhuria majadiliano ya Baraza la Haki za Binadamu (HRC) mjini Geneva, kuzingatia haki za wanawake kwamba bila ya kuwepo sheria za kuwakinga wanawake na mateso, pamoja na utumiaji mabavu dhidi yao, serikali za kimataifa na wote waliodhaminiwa madaraka ya utawala hawatofanikiwa kutekeleza usawa wa kijinsia kuimarisha maendeleo yao:~~