ICC inaishtumu Sudan kwa makosa ya jinai Darfur
Baraza la Usalama limekutana kwenye kikao cha hadhara kuzingatia suala la Darfur. Luis-Moreno Ocampo, Mwendesha Mashitaka wa Mahakama ya Kimataifa Juu ya Makosa ya Jinai ya Halaiki (ICC) alitarajiwa kuwakilisha ripoti maalumu yenye tuhuma zinazolenga wenye madaraka Sudan dhidi ya ukiukaji wa haki za binadamu katika Darfur.