Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Sikukuu ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani itaadhimishwa Mei tatu

Sikukuu ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani itaadhimishwa Mei tatu

Tarehe 03 Mei huadhimishwa kila mwaka na jamii ya kimataifa kuwa ni SikuKuu ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani. Idara ya Habari kwa Umma ya UM (DPI) pamoja na Shirika la UM juu ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) yameandaa tafrija mbalimbali kuwakumbusha walimwengu juu ya umuhimu, na pia ulazima, wa kuwa na vyombo vya habari vilivyo huru.