Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

BU kupitisha azimio kwa UNMIS kuendeleza shughuli za amani Sudan

BU kupitisha azimio kwa UNMIS kuendeleza shughuli za amani Sudan

Baraza la Usalama limepitisha maazimio kadha yanayohusu shughuli za ulinzi wa amani katika Bara la Afrika.~Awali, Ijumatano wajumbe wa Baraza la Usalama walipitisha, kwa kauli moja, azimio lilioahidi kuendelea kuunga mkono Mapatano ya Jumla ya Amani ya 2005 ya kusitisha uhasama, kati ya Sudan kaskazini na kusini, maafikiano ambayo utekelezaji wake unasimamiwa na kufuatiliwa na Shirika la UM la Ulinzi wa Amani Sudan Kusini (UNMIS). Azimio limependekeza shughuli za UNMIS ziendelezwe Sudan mpaka Aprili 30, 2009.