Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Siku ya Kumbukumbu ya Mauaji ya Rwanda kuheshimiwa Makao Makuu

Siku ya Kumbukumbu ya Mauaji ya Rwanda kuheshimiwa Makao Makuu

Leo magharibi, tarehe 07 Aprili KM wa UM Ban Ki-moon atatoa risala maalumu ya kuwakumbuka wale raia walioangamizwa Rwanda miaka 14 iliopita kutokana na jinai ya mauaji ya halaiki. KM anatarajiwa kuikumbusha jumuiya ya kimataifa kuhusu dhamana ya maadili waliokabidhiwa nayo na umma, ya kuunga mkono, kwa kauli moja, juhudi za UM za kuzuia janga karaha la mauaji ya halaiki kuibuka tena ulimwenguni. Kwa mujibu wa takwimu za UM watu 800,000 ziada waliangamia Rwanda na waathiriwa kadha wengineo walionusurika na mauaji walidhurika kiakili. KM ameahidi ya kuwa ataendelea kutumia muda wa utumishi wake katika UM kuhakikisha walimwengu tunafanikiwa kuuzuia milele hatari ya mauaji ya halaiki kuibuka tena duniani.