Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza la Haki za Binadamu laanza mapitio ya haki katika nchi 16

Baraza la Haki za Binadamu laanza mapitio ya haki katika nchi 16

Kikao cha awali cha Tume ya Utendaji ya Baraza la Haki za Binadamu imeanzisha ukaguzi maalumu, utakaoendelea hadi tarehe 18 Aprili, ambapo nchi wanachama 16 zitatathminiwa namna zinavyotekeleza haki za binadamu kwa raia zao. Miongoni mwa mataifa ya Afrika yatakayochunguzwa katika kikao hiki hujumuisha Algeria, Morocco, Tunisia na pia Afrika ya Kusini.