Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hali Darfur ni ya kutisha miaka minne baada ya vurugu kuzuka

Hali Darfur ni ya kutisha miaka minne baada ya vurugu kuzuka

Taarifa iliotolewa mwisho wa wiki kuhusu hali katika eneo la Sudan magharibi la Darfur ilimnakili KM Ban Ki-moon akisema tangu Baraza la Usalama lilipoanza kuzingatia vurugu liliozuka eneo hilo miaka minne iliopita, hali huko ni bado ya kutisha na inaendelea kuharibika hivi sasa.