Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNICEF yasaidia waalimu Zimbabwe kudhibiti UKIMWI

UNICEF yasaidia waalimu Zimbabwe kudhibiti UKIMWI

Waalimu 1,500 wa skuli za msingi na sekandari nchini Zimbabwe walishiriki kwenye mafunzo maalumu ya wiki moja kwa lengo la kuilimisha wanafunzi 500,000 juu ya taratibu kinga dhidi ya hatari ya kupatwa na VVU na UKIMWI. Mafunzo haya yaliweza kufanyika kutokana na msaada wa dola 500,000 uliofadhiliwa na Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF).