Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maendeleo Sudan kusini kuleta marekibisho kwenye operesheni za WFP

Maendeleo Sudan kusini kuleta marekibisho kwenye operesheni za WFP

Shirika la Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limeripoti kuwa itaanza kupunguza polepole operesheni za kuhudumia misaada ya dharura Sudan ya kusini, na badala yake kuanzisha miradi mipya ya muda mrefu ya kufufua kilimo, kwa sababu viashirio vimethibitisha mahitaji ya misaada ya kihali mwaka huu yatateremka kwa khumsi moja.