Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Washindi wa tuzo ya UNFPA mwaka 2016 watuzwa

Washindi wa tuzo ya UNFPA mwaka 2016 watuzwa

Wiki hii, mnamo Alhamis Juni 23, imefanyika hafla maalum kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, ya kutoa tuzo ya Shirika la Mfuko wa Idadi ya Watu (UNFPA) kwa washindi wa mwaka 2016.

Tuzo hiyo ya kila mwaka hutolewa kwa mtu binafsi na shirika au taasisi inayojikita katika kuboresha afya ya uzazi kwa wanawake, pamoja na afya ya akina mama na wajawazito.

Washindi wa mwaka huu wamebainishwa kwenye hafla iliyoghubikwa kwa muziki na shangwe. Kujua washindi hao ni akina nani, ungana na Assumpta Massoi katika makala hii.