Wakenya tulibisha hodi UM ili tupate uhuru : Macharia
Wakati shughuli mbali mbali zimepangwa kufanyika leo kuelekea kilele cha miaka 70 ya Umoja wa Mataifa ikiwemo tamasha la muziki kutoka kwa watumbuizaji wa Korea Kusini jijini New York, Kenya imesema bila ya Umoja wa Mataifa mchakato wa kupata uhuru na hatimaye maendeleo, ungekuwa mgumu. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
(Taarifa ya Assumpta)
Balozi Macharia Kamau ambaye ni mwakilishi wa kudumu wa Kenya kwenye Umoja wa Mataifa ameieleza idhaa hii kuwa Umoja hio sio tu umechangia miradi ya kimaendeleo bali pia katika usalama na amani lakini kubwa ziadi kwa Kenya ni.
(SAUTI KAMAU)
Amesema kila taifa linahitaji Umoja wa Mataifa ili liendelee kwani hakuna nchi inayoweza kujitiosheleza yenyewe.