Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vijana kusongesha Agenda 2030 ya malengo ya maendeleo endelevu - Monicah Malith

Monicah Malith, mmoja wa vijana waliofika kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kuhudhuria Jukwaa la Kisiasa la Ngazi za Juu la Umoja wa Mataifa (HLPF) mwaka 2024, akizungumza na Anold Kayanda wa Idhaa ya Kiswahili.
UN News
Monicah Malith, mmoja wa vijana waliofika kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kuhudhuria Jukwaa la Kisiasa la Ngazi za Juu la Umoja wa Mataifa (HLPF) mwaka 2024, akizungumza na Anold Kayanda wa Idhaa ya Kiswahili.

Vijana kusongesha Agenda 2030 ya malengo ya maendeleo endelevu - Monicah Malith

Malengo ya Maendeleo Endelevu

Jukwaa la kisiasa la ngazi ya juu la Umoja wa Mataifa HLPF, kuhusu malengo ya maendeleo endelevu SDGs limefikia tamati wiki iliyopita hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa  ambapo wawakilishi mbalimbali kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wamebadilishana uzoefu kwa takriban wiki mbili kuhusu jinsi ya kusongesha malengo hayo endelevu. Vijana nao hawakuachwa nyuma. 

Miongoni mwao ni Monicah Malith kutoka Kenya ingawa asili yake ni Sudan Kusini ambako alipakimbia akiwa na umri wa miaka 12 na sasa ni mwanafunzi wa sheria katika Chuo Kikuu cha Nairobi. 

Monicah anaeleza anazoziona ni changamoto za vijana kutoshiriki kikamilifu katika kuyafanikisha malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs katika kipengele cha mada kwa kina.