Nchini Ukraine, mashambulizi dhidi ya maeneo ya shule yameongezeka mara nne katika robo ya kwanza ya mwaka huu ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka jana, imesema taarifa iliyotolewa leo huko Kiev, Ukraine na New York, Marekani ikiongeza kuwa matukio hayo yamesababisha kiwewe kwa wanafunzi na kuwatia hatarini kupata majeraha au kuuawa.