UNHCR: Mamilioni ya wakimbizi wakabiliwa na baridi kali huku msaada wa kibinadamu ukipungua
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR limeonya leo kwamba wakati viwango vya joto vikianza kushuka katika maeneo mengi duniani, mamilioni ya wakimbizi na watu waliolazimika kuyakimbia makazi yao ndani ya nchi zao wanakabiliwa na majira ya baridi kali bila msaada wa kutosha, kufuatia kuporomoka kwa ufadhili wa kibinadamu.