Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ukraine

Nguo zenye joto na vifaa vingine vinagawiwa kwa familia zilizofurushwa huko Babekkeh, Syria.
© UNHCR/Hameed Maarouf

UNHCR: Mamilioni ya wakimbizi wakabiliwa na baridi kali huku msaada wa kibinadamu ukipungua

Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR limeonya leo kwamba wakati viwango vya joto vikianza kushuka katika maeneo mengi duniani, mamilioni ya wakimbizi na watu waliolazimika kuyakimbia makazi yao ndani ya nchi zao wanakabiliwa na majira ya baridi kali bila msaada wa kutosha, kufuatia kuporomoka kwa ufadhili wa kibinadamu.

Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine akihutubia mjadala mkuu wa kikao cha themanini cha Baraza Kuu.
UN Photo/Loey Felipe

Ukraine: Taasisi za kimataifa zimekuwa dhaifu

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy amesema taasisi za kimataifa zimekuwa dhaifu wanachoweza kufanya ni kutoa matamko makali pekee na kwamba kwa sasa duniani sheria pekee za Kimataifa haziwezi kusaidia nchi kujilinda bila ya kuwa na silaha pamoja na marafiki wenye nguvu wa kukusaidia. 

Sauti
3'4"
© UNICEF/Oleksii Filippov

Taasisi za kimataifa zimekuwa dhaifu - Volodymyr Zelenskyy

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy amesema taasisi za kimataifa zimekuwa dhaifu wanachoweza kufanya ni kutoa matamko makali pekee na kwamba kwa sasa duniani sheria pekee za Kimataifa haziwezi kusaidia nchi kujilinda bila ya kuwa na silaha pamoja na marafiki wenye nguvu wa kukusaidia. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.

Sauti
3'4"

24 SEPTEMBA 2025

Hii leo jaridani tunaangazia hotuba ya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy katika siku ya pili ya mjadala mkuu wa UNG80, na ujumbe wa washiriki wa mkutano huu kutoka Nigeria na Tanzania.

Sauti
9'59"
Mabomu yanayolipuka na kusambaza vilipuzi vingine yanawezakuwa yalitumika Ukraine.
© UNOCHA/Adedeji Ademigbuji

Mabomu yanayolipuka na kusambaza vilipuzi vingine  yameua na kujeruhi mamia ya raia nchini Ukraine tangu mwaka 2022: UNIDIR

Mabomu yanayolipuka na kusambaza vilipuzi vingine  yameua na kujeruhi zaidi ya raia 1,200 nchini Ukraine tangu kuanza kwa uvamizi mkubwa wa Urusi mwezi Februari 2022, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na muungano wa mashirika yasiyo ya kiserikali unaoungwa mkono na Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Utafiti wa Udhibiti wa Silaha UNIDIR.