06 MACHI 2020
Katika Jarida letu leo la mada kwa kicha Grace Kaneiya anakuletea
Miaka 25 baada ya jukwaa la Beijing la kuchukua hatua kuhusu Haki za wanawake, Umoja wa Mataifa unasema wakati ni sasa na hakuna kinachohalalisha kutokuwepo kwa usawa wa kijinsia
-Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limeona zaidi ya dola milioni 260 kwa ajili ya kuwasaidia wakimbizi wa DRC walioko nje na jamii zinazowahifadhi
-Kamishina Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Michelle Bachelet amesisitiza kuwa hatua zozote zinazochukuliwa kukabiliana na mlipuko wa COVID19 zihakikishe hazikiuki haki za binadamu
-Mada kwa kina leo tuikielekea siku ya wanawake duniani inatupeleka Shinyanga Tanzania utakutana na mama anayeponda kokoto ili kujikimu yeye na familia yake
-Kama ada ya kila Ijumaa ni kujifunza Kiswahili na leo mchambuzi wetu Onni Sigalla mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili Tanzania BAKITA anachambua maana ya neno "PANJA"