Mbinu za kukabiliana na ukimwi nchini Uganda
Pakua
Wakati siku ya ukimwi duniani imeadhimishwa leo Disemba mosi huhu kukitajwa baadhi ya mafanikio yaliyopatikana hadi sasa, bado kuna changamoto kadhaa ambazo zinakwamisha lengo la kutokomeza kabisa ukimwi . Mathalani upatikanaji wa huduma na tiba kwa wale wanaoishi na virusi vya Ukimwi. Hata hivyo nchi mbali mbali zimechukua hatua kuhakikisha kwamba vita dhidi ya ukimwi vinaendelezwa miongoni mwa nchi hizo ni Uganda. Je nini kinafanyika? Basi ungana na John Kibego wa Radio washirika ya Spice fm nchini humo.