Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Misri yataka makubaliano mapya kuhusu matumizi ya mto Nile

Misri yataka makubaliano mapya kuhusu matumizi ya mto Nile

Pakua

Nchi saba zitumiazo maji ya mto Nile, miaka michache iliyopita zilianzisha mkataba mpya unaotaka kuwepo kwa uwiano sawa wa matumizi ya maji ya mto Nile.

Waziri wa mambo ya Nje wa Misri Mohamed Kamel Amr hivi sasa ameanza safari ya kuzitembelea nchi hizo saba kwa ajili ya kuweka ushawishi kabla mkutano wao wiki ijayo Nairobi Kenya.

Kwa mujibu wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania Bwana Bernard Membe, kuna uwezekano sasa pande hizo zikafikia makubaliano yatayozingatia maslahi ya pande zote. George Njogopa anaripoti

(PKG YA GEORGE NJOGOPA)