WFP inasaka fedha kuendelea kuwasaidia waathirika wa Kimbunga Mocha
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) linasema hadi kufikia mwisho wa mwaka huu 2023 linahitaji dola za Marekani milioni 60 ili kutoa msaada wa chakula cha kuokoa maisha nchini Myanmar kwa watu milioni 2.1 walioathiriwa na majanga mengi na magumu kikiwemo kimbunga Mocha.