Ecuador yakosolewa kwa kukandamiza haki
Wataalam maalum wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu wameikosoa serikali ya Ecuador kwa jinsi inakandamiza haki za kiraia kufuatia kitendo chake cha kuamuru kufungwa kwa shirika la kiraia linalotetea haki za watu wa asili na mazingira.