Ukatili na mauaji vyaendelea Sudani Kusini- Ripoti
Ripoti ya watalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa iliyotolewa wiki hii imesema baada ya miaka minne ya machafuko nchini Sudan Kusini imebanika kuwepo kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na pande kinzani uliosababisha maisha ya watu wengi wasio na hatia kupotea.