Umoja wa Mataifa walaani mauaji nchini Nigeria
Umoja wa Mataifa walaani mauaji nchini Nigeria
Amani na Usalama
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali mashambulizi ya kutisha yaliyotekelezwa mwishoni mwa juma katika Jimbo la Zamfara nchini Nigeria ambapo raia wengi waliuawa.
Guterres ametuma salamu za rambirambi kwa familia zilizofiwa kwenye shambulio hilo.
Katibu Mkuu pia amezitaka mamlaka za Nigeria kuhakikisha zinafanya juhudi zote ili kuwapata na kuwafikisha mahakamani wale wote waliohusika na uhalifu huo mbaya.
Umoja wa Mataifa inaunga mkono na kuonesha mshikamano na serikali ya Nigeria katika mapambano na vita dhidi ya ugaidi, itikadi kali za kikatili na uhalifu uliopangwa.