Raia 25 wameuawa Oicha DRC wiki hii na wengine kadhaa kujeruhiwa:UN
Machafuko yanayoshika kasi katika jimbo la Kivu ya Kaskazini Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, yameendelea kukatili Maisha ya watu , kujeruhi na kuwalazimisha wengi kufungasha virago na kuzikimbia nyumba zao kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.