Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

mauaji

Shule ya Al-Imam Al-Kadhim kwenye mji wa Al-Geneina jimbo la Darfur Magharibi nchini Sudan, ambayo imekuwa hifadhi kwa wakimbizi wa ndani iliteketezwa kwa moto wakati huu ambapo mapigano yanaendelea nchini Sudan.
© Mohamed Khalil

OHCHR: Makaburi ya watu wengi yagunduliwa nchini Sudan

Miili ya takriban watu 87 ya kabila la Masalit na wengine wanaodaiwa kuuawa mwezi uliopita na vikosi vya msaada wa haraka RSF na washirika wao huko Darfur Magharibi nchini Sudan, imezikwa kwenye kaburi la pamoja huko El-Geneina kwa amri ya vikosi hivyo kulingana na taarifa za kuaminika ambazo Ofisi ya Haki za Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa imezipata. 

UNHCR Video

OHCHR yapokea ripoti za raia kuuawa na wanawake kubakwa nchini Sudan

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya haki za binaadamu, OHCHR imeeleza kusikitishwa na athari mbaya za mapigano kwa raia zinazoendelea nchini Sudan ambapo mpaka hizi sasa wamepokea taarifa za kuuawa kwa raia ikiwemo watoto na wajawazito na ubakaji huku waandishi wa habari wakiwa katika hali mbaya kutokana na kauli za chuki hususani mitandaoni.

Akizungumza na waandishi wa habari hii leo jijini Geneva Uswisi msemaji wa Ofisi hiyo ya Haki za Binadamu Jeremy Laurence amesema, 

Sauti
2'13"
Wakimbizi kutoka Sudan wakisubiri kupokea vifaa muhimu vya msaada kakati wa usambazaji huko Koufroun, kijiji cha Chad karibu na mpaka wa Sudan.
© UNICEF/Donaig Le Du

Ofisi ya Haki za Binadamu ya UN yapokea ripoti za raia kuuawa na wanawake kubakwa nchini Sudan

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya haki za binaadamu, OHCHR imeeleza kusikitishwa na athari mbaya kwa za mapigano kwa raia zinazoendelea nchini Sudan ambapo mpaka hizi sasa wamepokea taarifa za kuuawa kwa raia ikiwemo watoto na wajawazito, ubakaji huku waandishi wa habari wakiwa katika hali mbaya kutokana na matamshi ya chuki hususani mitandaoni.

Sauti
2'13"
UNICEF/Karel Prinsloo

Wanafunzi nchini Nigeria wahitaji ulinzi zaidi: UNICEF

Ikiwa ni miaka tisa imepita tangu wasichana 276 kutekwa nyara wakiwa katika shule ya bweni huko Chibok Nigeria ambapo mpaka sasa 96 bado wapo utumwani, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limetaka wadau kusaidia katika kuwekeza zaidi katika usalama wa wanafunzi mashuleni kwani bado vitendo vya utekaji vinaendelea nchini humo.

Sauti
2'14"
Mlinzi wa amani wa UNMISS nchini Sudan Kusini akishika doroa kwenye jimbo la Equatorial
UN Photo/Isaac Billy

Raia wa Sudan Kusini walikatiliwa na kuuawa Zaidi mwaka 2022 ikilinganishwa na 2021: UNMISS

Mpango wa umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini UNMISS leo umetoa taarifa ya kila mwaka ya haki za binadamu na ukatili unaoatjiri raia ambayo inaonyesha kuna ongezeko la asilimia 2 la idadi ya raia waliokatiliwa nchini humo mwaka 2022, licha ya kupungua kwa vitendo vya ukatili kwa ujumla kwa asilimia 27 mwaka 2022 ikilinganisha na mwaka 2021.

Mwanamke akishiriki katika maandamano ya kupinga ukatili wa kijinsia huko Quito, Ecuador.
© UN Women/Johis Alarcón

Wanawake na wasichana ndio walio hatarini zaidi kuuawa majumbani: UN Women/UNODC

Ripoti ya utafiti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake UN Women na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya madawa na uhalifu UNODC inaonyesha kuwa wanawake na wasichana ndio walio katika hatari kubwa ya kuuawa majumbani, ikionyesha kuwa kwa wastani zaidi ya wanawake au wasichana watano waliuawa kila saa na wenzi wao au jamaa wa familia kwa mwaka 2021. 

Sauti
3'33"