UNICEF yalaani shambulio lililoua watoto 17 Kaskazini mwa Darfur Sudan
Watoto wasiopungua 17 wasichana tisa na wavulana wanane, akiwemo mtoto mchanga wa siku saba wameuawa katika shambulio lililotokea katika kituo cha wakimbizi wa ndani cha Dar al-Arqam mjini El Fasher, Kaskazini mwa Darfur, mapema Jumamosi asubuhi, kwa mujibu wa taarifa zilizopokelewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF.