Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

mauaji

Watoto wameketi nyuma ya lori huku familia zikifurushwa tena na vita huko Gaza.
© UNICEF/Eyad El Baba

Fletcher: Msaada lazima uende mahali ambapo mahitaji ni makubwa zaidi huko Gaza

Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limekutana hii leo jijini New York Marekani katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kujadili kuongezeka kwa mzozo wa kibinadamu huko Gaza, ambako amri mpya za kuwataka watu kuhama katika makazi yao zinazotolewa na jeshi la Israel zimewaondoa makumi kwa maelfu ya watu walati huo huo mashambulizi ya mabomu yakendelea kukatisha uhai wa watu wakiwemo watoto.

Wapalestina ambao wamekimbilia shule ya UNRWA katika kambi ya Deir al-Balah katikati mwa Gaza wanatatizika kuishi huku wakikosa huduma za kimsingi za kibinadamu katika mji wa kati wa Gaza wa Deir al-Balah.
© UNRWA/Louise Wateridge

Wapalestina wanalazimika kuuawa ili kulisha familia zao Gaza, UN yataka uchunguzi wa haraka

Dunia inashuhudia kila siku "mandhari ya kutisha ya Wapalestina kupigwa risasi, kujeruhiwa au kuuawa huko Gaza wakiwa wanajaribu tu kupata chakula," amesema Mratibu Mkuu wa Misaada ya Kibinadamu na masuala ya Dharura wa Umoja wa Mataifa, Tom Fletcher, akisisitiza wito wake wa kuruhusu Umoja wa  Mataifa kutekeleza jukumu lake la kutoa msaada wa kuokoa maisha.

Duka la muda huko Gaza, ambapo mashambulizi ya mabomu yanayoendelea ya Israel yameharibu au kuharibu majengo 170,812 - au asilimia 69 ya jumla ya majengo yote kwa mujibu wa UNOSAT.
© UNFPA/Media Clinic

Mvua, msimu wa baridi na vizuizi vya misaada vinazidisha mateso kwa watu milioni moja Gaza: UN

Takriban watu milioni moja wa Gaza wanakabiliwa na hatari ya kuishi majira ya baridi bila makazi ya kutosha huku mashirika ya Umoja wa Mataifa yakihaha kutoa msaada wa kukabiliana na hali ya hewa ya baridi, wakati kukiwa na mashambulizi yanayoendelea ya Israel, maagizo ya mara kwa mara ya watu kuhama na vikwazo vya kuwasilisha misaada, yameonya leo mashirika ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa.