COVID-19 imeongeza pengo la usawa wa kijinsia kwa wakimbizi wanawake na wasichana:UNHCR
COVID-19 imeongeza pengo la usawa wa kijinsia kwa wakimbizi wanawake na wasichana:UNHCR
Athari za janga la COVID-19 zinatishia maisha na haki za wakimbizi, wanawake na wasichana wasio na makazi, limeonya leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi NHCR, wakati ikiadjimishwa Siku ya wanawake duniani.
Kamisha mkuu wa UNHCR Filipo Grandi amesema “Athari hizo ambazo ni za kiuchumi na kijamii hazijawahi kutokea na zinayaacha Maisha ya watu wengi katika hatari kubwa.Tunashuhudia kuongezeka kwa ripoti za unyanyasahji wa kijinsia, pamoja na unyanyasaji wa majumbani, ndoa za kulazimishwa, utumikishwaji wa watoto na mimba za utotoni.” Hizi zinahusishwa na kuongezeka kwa shinikizo za kijamii na kiuchumi, kuongezeka kwa mivutano katika majumbani na katika jamii na kufungwa kwa shule, zote zikisababishwa na umaskini unaohusiana na janga la COVI-19. Ameongeza Bwana Grandi. Pia amesema baadhi ya manusura hata wanaamua kuchukua hatua kali ya kuondoa malalamiko yao kwa sababu ya utegemezi wa kiuchumi kwa wenzi wanyanyasaji. Pengo la usawa linapanuka"Tunashuhudia dhihirisho kubwa la ukosefu wa usawa wa kijinsia kwa baadhi ya watu walio katika mazingira hatarishi zaidi na walio katika mazingira magumu na mmomonyoko wa kutisha wa hatua muhimu zilizokwishapigwa katika usawa wa kijinsia miongo michache iliyopita," amesema Grandi. Ameongeza kuwa “Jumuiya ya kimataifa lazima ichukue hatua na kusaidia kulinda haki za wanawake na wasichana waliolazimika kutawanywa na wasio na utaifa. Hii inahitaji msaada kwa mipango ya kibinadamu inayopambana na pengo la usawa wa kijinsia, ikiwemo unyanyasaji wa kijinsia, na pia kuongeza wigo wa elimu, mipango ya ufundi na kujitegemea. Ni muhimu kwamba wanawake na wasichana hao pia wajumuishwe katika mipango ya misaada ya kijamii na kiuchumi inayowekwa na kutekelezwa na serikali. ” |
|
Asilimia 85 ya wakimbizi wote duniani wanahifadhiwa katika mataifa yanayoendelea na kwa kiasi kikubwa wanategemea misaada ya kibinadamu au vibarua vya kutwa. Wengi sasa wamepoteza uwezo wa kujimudu kimaisha na wametumbukizwa katika umasikini wa kutisha na athari mbaya na kubwa. "Pamoja na kuongezeka kwa hatari za machafuko, unyanyasaji, unyanyasaji wa kijinsia na usafirishaji haramu wa binadamu, vyote vikiwa ni matokeo ya kutokuwepo kwa usawa wa kijinsia, athari za janga la COVID-19 pia zinathibitisha maafa katika elimu ya wasichana wa wakimbizi. Wasichana wengi wanalazimika kuacha shule na kufanya kazi, kuuzwa au kuolewa, " kwa mujibu wa mkuu wa ulinzi wa UNHCR, Gillian Triggs. Wasicha milioni 13 hatarini kwa ndoa za utotoni UNHCR inasema wakati washirika wa masuala ya kibinadamu wanakadiria kuwa wasichana zaidi ya milioni 13 sasa wako katika hatari ya kuolewa kwa kulazimishwa kutokana na janga COVID-19, ndoa za utotoni tayari zinageukiwa na familia zingine za wakimbizi ambazo zimeghubikwa na kudhoofishwa na umasikini. Shirika hilo limeongeza kuwa wanawake wakimbizi pia wanaelemewa na mzigom wa kutoa huduma na utunzaji wa ziada majumbani, wakigeukia kazi za hatari katika sekta isiyo rasmi, au mitaani. Pia janga hilo la corona limeongeza mahitaji ya kaya na kunapunguza fursa zao za elimu nah uku wakiwa katika hatari kubwa ya maambukizi ya virusi hivyo. Triggs amesisitiza kwamba "Ulemavu, kutengwa, mwelekeo wao wa kijinsia na utambulisho wao wa kijinsia pia vinazidisha ubaguzi na hatari za unyanyasaji kwa wanawake na wasichana wakimbizi, wasio na makazi, waliotawanywa na wasio na utaifa." Ameongeza kuwa licha ya janga la COVID-19 kuchochea kukosekana kwa usawa wa kijinsia na kuongeza hatari za unyanyasaji dhidi ya wanawake na wasichana, mipango ya kuzuia na kukabiliana nao bado haijapata ufadhili wa kutosha. Kushiriki kikamilifu na kwa maana kwa wanawake na wasichana katika maamuzi ambayo yanaathiri maisha yao, familia na jamii zao ni muhimu katika kudumisha haki zao za binadamu, kuhakikisha ulinzi wao imara na kusaidia uwezeshwaji wao. "Hadi pale juhudi za pamoja zitakapofanyika kupunguza athari za kijinsia za COVID-19, tuna hatari ya kuwaacha nyuma wanawake na wasichana wakimbizi, waliotawanywa na wasio na uraia," amesema Triggs. |