Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mauaji yaliyotekelezwa kwenye hekalu yanaashiria chuki dhidi ya wayahudi-Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres  akihutubia kwenye sinagogi la Park East jijini New York, Marekani (31 Oktoba 2018)
UN /Rick Bajornas
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akihutubia kwenye sinagogi la Park East jijini New York, Marekani (31 Oktoba 2018)

Mauaji yaliyotekelezwa kwenye hekalu yanaashiria chuki dhidi ya wayahudi-Guterres

Amani na Usalama

Mauaji ya watu wawili nje ya hekalu nchini Ujerumani leo Jumatano yametajwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa  Antonio Guterres kama “tukio la kuashiria chuki dhidi ya waayahudi.”

Shambulio hilo kwenye mji wa Halle, mashariki mwa Ujerumani yalitokea katika siku kuu ya wayahudi ya Yom Kippur, ambayo ni siku takatifu kabisa kwenye mwaka wa wayahudi.

Bwan  Guterres kupitia taarifa ya msemaji wake iliyotolewa jijini New York, Mareknai amelaani vikali shambulizi hilo ambapo amesema matukio kama hayo yanahitaji kupingwa kwa nguzu zote.

Duru zinasema kwamba mtekelezaji wa shambulio hilo alikuwa amevali mavazi yanayofanana na sare za kijeshi na alikuwa na kamera ya kunasa video ambayo alikuwa akitumia kuonyesha mbashara mashambulizi hayo.