Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nakaribisha uamuzi wa Rais wa Cameroon kuanzisha majadiliano ya kitaifa:Guterres

Asubuhi katika mitaa ya Melen, mtaa wa mabanda katikati ya mji mkuu wa Cameroon, Yaoundé. Kwa muda mrefu Cameroon imekuwa katika mgogoro wa ndani.
UN-Habitat/Kirsten Milhahn
Asubuhi katika mitaa ya Melen, mtaa wa mabanda katikati ya mji mkuu wa Cameroon, Yaoundé. Kwa muda mrefu Cameroon imekuwa katika mgogoro wa ndani.

Nakaribisha uamuzi wa Rais wa Cameroon kuanzisha majadiliano ya kitaifa:Guterres

Amani na Usalama

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amekaribisha tangazo la rais Paul Biya wa Cameroon la kuanzisha mchakato wa majadiliano ya kitaifa.

Kupitia taarifa iliyotolewa na msemaji wake jumanne, Bwana Guterres ameichagiza serikali ya Cameroon kuhakikisha kwamba mchakato huo unakuwa jumuishi na kushughulikia changamoto zinazolikabili taifa hilo la afrika ya Magharibi.

Katibu Mkuu pia ametoa wito kwa wadau wote nchini Cameroon wakiwemo wanaoishi ughaibuni, kushiriki katika juhudi hizo.

Pia amerejelea kuhimiza kwamba Umoja wa Mataifa uko tayari kuisaidia Cameroon katika mchakato huo wa kitaifa wa majadiliano.