Hata kama wana matatizo ya kujifunza , elimu ni haki yao- Michael Okiro
Hata kama wana matatizo ya kujifunza , elimu ni haki yao- Michael Okiro
Leo ni siku ya ugonjwa unaoathiri uwezo wa kujifunza duniani au Down syndrome, ukiwa umebeba kaulimbiu “kutomuacha mtu yeyote nyuma kielimu” suala ambalo ni changamoto kubwa kwa nchi nyingi. Hata hivyo kwa mujibu wa shirika la afya duniani hatua zimeanza kuchukuliwa na baadhi ya mataifa kutimiza lengo la kuhakikisha watoto wanaozaliwa na matatizo uwezo wa kujifunza wanapata elimu. Uganda ni miongoni mwa nchini zilizopiga hatua kwa kuweka sharia za kuhakikisha elimu inatolewa bure kwa watu wenye ugonjwa huu.
Akizungumza na idhaa ya Umoja wa Mataifa kwa njia ya simu kutoka Kampala Uganda , Mkurugenzi wa taasisi ya Uganda ya watoto wanaozaliwa wakiwa na down Syndrome Dkt Michael Okiro Obwokor anafafanua kinachofanywa na serikali kuhakikisha hilo
(Sauti Ya Dkt Michael Okiro Obwokor)
Na kuhusu wajibu au jukumu la jamii na wazazi kuhakikisha watoto hao wanahamasishwa amesema ….
(Sauti Ya Dkt Michael Okiro Obwokor)