Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WHO yalaani shambulizi dhidi ya wahudumu wa afya Iraq

Wahudumu wa afya wakisaidiwa UNICEF wakiwa katika ziara ya mama aliyejifungua mwanae mchanga huko Iraq.
UNICEF/UN032140/Mackenzie
Wahudumu wa afya wakisaidiwa UNICEF wakiwa katika ziara ya mama aliyejifungua mwanae mchanga huko Iraq.

WHO yalaani shambulizi dhidi ya wahudumu wa afya Iraq

Sheria na Kuzuia Uhalifu

Shirika la afya duniani (WHO) limelaani vikali  shambulio la hivi karibuni dhidi ya muhudumu wa afya ambaye alishambuliwa wakati akitoa huduma kwamgonjwa mahtuti  ajuza wa miaka 70 katika Hospitali ya Azadi  iliyopo katika jimbo la Kirkuk mapema nchini Iraq tarehe 18 mwezi huu.

Dk. Adham Rashad Ismail, ambaye ni kaimu mratibu wa WHO Iraq amesema "Mashambulizi dhidi ya wahudumu wa afya ni ukiukwaji mkubwa wa sheria za kimataifa za kibinadamu na kuwanyima idadi kubwa ya watoto, wanawake na wazee  haki zao za huduma muhimu ya afya zinayotolewa na shirika hilo.”

Takwimu za WHO, zimebaini kuwa wahuduma   katika vituo vya afya nchini Iraq wamekuwa wakishambuliwa tangu mgogoro ulivyongezeka mwaka 2014. Mnamo 2018 pekee, mashambulizi 42  yalirekodiwa na WHO Iraq, na asilimia  40% kati ya hayo ni dhidi ya wahudumu wa afya nchini

WHO inatoa wito kwa mamlaka  nchini humo kuhakikisha usalama wa wafanyakazi na wa wahudumu wa afya katika vituo mbalimbali  vya afya, wakati huu ambapo idadi kubwa ya watu wakiwemo wakimbizi wa ndani , jumuiya za wenyeji na wahamiaji wanaendelea kuhitaji huduma muhimu, za kuokoa maisha,  na pia kuhakikisha wagonjwa na vituo vya afya vinalindwa.