Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vita visipokoma njaa itazidi kuwaangamiza Wayemen:WFP

Mkuu wa UNICEF kanda ya mashariki ya kati na Afrika kakskazini,Geert Cappelaere Geert, akikagua msaada wa kinadamu ukiwasili katika bandari ya Hodeidah , Yemen na pia msaada huo kuopakiwa kwenye  malori.
© UNICEF/Ahmed Abdulhaleem
Mkuu wa UNICEF kanda ya mashariki ya kati na Afrika kakskazini,Geert Cappelaere Geert, akikagua msaada wa kinadamu ukiwasili katika bandari ya Hodeidah , Yemen na pia msaada huo kuopakiwa kwenye malori.

Vita visipokoma njaa itazidi kuwaangamiza Wayemen:WFP

Msaada wa Kibinadamu

Kutokana na  kuzorota kwa hali ya kiusalama  nchini Yemen, shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani  WFP linataka mapigano ya sasa katika mji wa bandari wa Hodeidah yakomeshwe mara moja kwani mbali ya kukatili Maisha ya watu yanayongeza idadi ya waathirika wa njaa linalowapa msaada wa chakula ,iliyopanda kutoka milioni 8  hadi milioni 14.  

Katika barabara za mji wa Hodeidah uliosal;ia mahame nakujawa na vizuizi kadhaa  barabarabani watu wengi wamefungasha virago kukimbia machafuko.

Kwa muda sasa mji wa Hodeidah umekuwa uwanja wa mapambano  huku mahandaki yakionekana bayana barabarani . Hadi kufikia Juni mwaka huu wa 2018, takriban nusu milioni walikuwa wameuhama mji huo na wale walio baki maisha yao yako mashakani kutokana na mapigano yanayoendelea.

Bandari hiyo ndiyo uti wa mgongo wa Yemen kwani ndiyo njia pekee ya kuingizia chakula na mafuta ukizingatia kwamba  asilimia 90 ya chakula cha Yemen kinatoka nje.  Amer Daoudi ni Mkurugenzi mkuu wa operesheni wa WFP.

"Hodeidah inauwezo  wa kumudu takriban asilimia 70 ya bidhaa zote zinzoingia Yemen kutoka nje  , na endapo fursa hiyo haitokuwepo tutashuhudia zahma nchini Yemen na maisha ya watu yatakuwa hatarini . WFP inaongeza juhudi ili kuweza kutimiza mahitaji ya watu milioni 14 na Hodeidah ndiyo njia pekee muhimu kwetu kuweza  kutimiza mahitaji ya watu hao.”

 Na watoto wa Hodeidah ambako ndiko kwenye kiwango cha utapia mlo, wakati mwingine huwa dhaifu hata hushindwa kufungua vinywa kula chakula maalum wanachopewa kwa ajili ya kuimarisha lishe na siha yao.

Hivi sasa  WFP inalenga kutoa chakula cha msaada kwa watu milioni 8 na bajeti yake ya dola milioni125 kwa mwezi itakuwa mtihani mgumu endapo fedha zaidi hazitopatikana kuhakikisha huduma hiyo ya lazima ya chakula inapatikana kwa maelfu ya watu wanaokabiliwa na njaa.