Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabilioni ya barua na vifurushi bado yanategemea posta kila mwaka:UPU

Kuchambua barua
Universal Postal Union
Kuchambua barua

Mabilioni ya barua na vifurushi bado yanategemea posta kila mwaka:UPU

Masuala ya UM

Posta bado ina mchango mkubwa kote duniani  kwa maisha ya watu na maendeleo endelevu ambapo kila mwaka husafirisha barua bilioni 368.4 na vifurushi bilioni 6.4

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, katikakuadhimisha siku ya Posta duniani ambayo kila mwaka huwa Oktoba 9.

Katika ujumbe wake kwa siku hii, Bw Guterres, amesema sekta ya Posta ambayo ina ofisi zaidi ya 600,000 duniani kote, ni moja ya vituo vyenye mtandao mkubwa duniani ambao ni muhimu kwa maisha ya jamii.

Amesema kuwa maadhimisho ya mwaka huu, ni ishara ya thamani ya sekta hiyo sio tukatika kusafirisha barua tu  lakini pia mizigo.

Mfumo wa posta uliothabiti, amesema Katibu Mkuu hutoa msaada wakati wa majanga, pia hutoa huduma za kifedha kwa mamilioni ya watu, na hutoa habari muhimu kwa watu hususan  wakati wa migogoro.

Ameongeza kuwa mtandao huu, ni sauti ya ushirika na pia chombo cha msukumo wa ajenda ya 2030 ya maendeleo endelevu ikiwa ni pamoja na kusaidia kukuza  usomaji na elimu kwa watoto.

Kwa upande wake, mkurugenzi mkuu wa  ofisi ya kimataifa ya Muungano wa Posta duniani UPU- Bishar A. Hussein, anasema, kila siku duniani kote huduma za posta zinachangia kitu kipya katika maisha ya watu na jamii. Hii ni kutokana na utoaji wake  wa huduma muafaka, za bei nafuu  na zenye kuaminika duniani kote.

 Posta husafirisha barua bilioni 368.4 na vifurushi bilioni 6.4 kila mwaka.
Photo: Universal Postal Union (UPU)
Posta husafirisha barua bilioni 368.4 na vifurushi bilioni 6.4 kila mwaka.

 

Ameongeza kuwa posta ni daraja la kuiunganisha jamii kwa  kuhakikisha  wananchi wote wanapata huduma kupitia mitandao yake  hata na wale waishio katika sehemu za mashambani, katika visiwa na pia katika maeneo yenye majanga.

Na kwa watu wengi amesema posta ndio chombo pekee cha kuelimika kwa kupata habari kuhusu afya na usalama.

Pia amesema katika enzi ya sasa ya kidigitali, Posta imejiweka katika nafasi ya mchangiaji mkuukwenye ulimwengu wa biashara ya mtandao yaani e-commerce.

Kauli mbiu yam waka huu ni ‘Posta hutoa hutoa huduma bora kwa dunia”.

UPU iliundwa mwaka 1874 na makao yake makuu yako Berne Uswisi. Na ndiyo shirika lisilo la kiserikali kongwe zaidi duniani na limekuwa chini ya mwamvuli wa Umoja wa Mataifa tangu mwaka 1948. Duniani kote kuna wafanyakazi wa Posta wapatao milioni tano, na ofisi 663,000 katika nchi 192.