Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uhamiaji sio shida Afrika la msingi kutovunja sheria- Rais Nyusi

Rais wa Msumbiji, Filipe Jacinto Nyusi
Daniela Gross
Rais wa Msumbiji, Filipe Jacinto Nyusi

Uhamiaji sio shida Afrika la msingi kutovunja sheria- Rais Nyusi

Wahamiaji na Wakimbizi

Suala la uhamiaji likiendelea kuibua vuta nikuvute, Msumbiji imesema kuwa la msingi ni watu kufuata sheria kwani uhamiaji umekuwepo na utaendelea kuwepo.

Uhamiaji sio mzigo wala shida, unageuka kuwa shubiri pale sheria zinapovunjwa au watu kuitumia vibaya fursa hiyo kwa vitendo vya kihalifu. John Kibego na taarifa kamili

Kauli hiyo imetolewa na Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi  alipozungumza na idhaa ya Kiswahili wakati wa mjadala wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaoendelea mjini New York Marekani  na kujadili nada mbalimbali ikiwemo uhamiaji.

Rais Nyusi ambaye pia ameishukuru serikali ya Kenya kwa kuwakumbatia raia wa Msumbiji waliokuwa wahamiaji wa miaka mingi nchini humo amesema Afrika hivi sasa imebadilika na kuwa na mtazamo chanya kuhusu uhamiaji na faida zake.

 

UN News/Grace Kaneiya
UNGA73- Rais Felipe Nyusi, Msumbiji

Ameongeza kuwa hata nchi yake haijafunga mipaka wala milango kwa wahamiaji

(SAUTI YA RAIS FILIPE NYUSI )