Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Msumbiji

© UNICEF/UNI404964/Zuniga

Madarasa yajengwa Sofala, Msumbiji kuhimili majanga ya asili ikiwemo vimbunga

Hii leo Umoja wa Mataifa umetoa ripoti ya kwanza ya uchambuzi wa aina yake kuhusu matukio ya watoto kulazimika kukimbia makwao kutokana na majanga yasababishwayo na hali ya hewa ikisema zaidi ya watoto milioni 43 walijikuta wakimbizi wa ndani kwenye nchi 44 katika kipindi cha miaka sita iliyopita, ikitafsiri kuwa ni watoto 20,000 kila siku.

Makadirio ya ripoti hiyo ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, yanaonesha kuwa kufurika kwa mito pekee kutafurusha watoto milioni 96 katika miaka 30 ijayo.

Sauti
4'41"

21 AGOSTI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia Siku ya waathirika wa ugaidi duniani na mabomu ya kutegwa ardhini. Makala tunakupeleka nchini Siarra Leone na mashinani nchini Msumbiji, kulikoni? 

Sauti
9'56"
© UNICEF/Jean-Claude Wenga

UNICEF: Watoto katika nchi 11 za Mashariki na Kusini mwa Afrika wako hatarini sababu ya kipindupindu

Nchi 11 Mashariki na Kusini mwa Afrika zinakabiliwa na hali mbaya ya mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ambako hadi sasa kumeripotiwa wagonjwa 67,822 na vifo 1, 788 kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF.

Taarifa ya UNICEF iliyotolewa leo mjini Nairobi, Johannesburg na New york inasema huenda idadi kamili ya wagonjwa na vifo ikawa kubwa zaidi kutokana na changamoto ya mifumo ya ufuatiliaji, utoaji taarifa na unyanyapaa.

Sauti
2'21"