UNHCR yapongeza Ukrane kwa kupitisha pensheni ya wakimbizi wa ndani
Mahakama kuu zaidi nchini Ukraine imetoa uamuzi unaosaidia mamia kwa maelfu ya wazee, wakimbizi wa ndani na wakaazi katika maeneo yasiodhibitiwa na serikali kupata pensheni zao ambazo wamekosa tangu 2014.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, limefurahia uamuzi huo wa tarehe 4 Septemba ukisema kama ni hatua muhimu katika kufuta machozi kwenye macho ya waathirika wa mgogoro wa miaka mitano nchini Ukraine ambao kwa sasa wako katika uhitaji mkubwa wa msaada.
Mkurugenzi wa UNHCR, Ulaya Pascale Moreau, akiipongeza Ukraine kwa hatua hiyo adhimu, amewaimba mamlaka ya nchini hiyo kuhakikisha kwamba uamuzi huo umetekelezwa haraka iwezekanavyo ili kutuliza nyoyo za watu wanaotegemea penshehi kupata mahitaji ya msingi.
Sasa ni miaka mitano mapigano yakiendelea kuibua madhila kwa maelfu ya watu mashariki mwa Ukraine.
Kwa mantiki hiyo, UNHCR imepaza tena sauti yake ikiiomba jamii ya kimataifa kuendeleza msaada kwa watu milioni 3.4 wanohitaji msaada wa kibinadamu.