Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Malawi chunguzeni vitisho dhidi ya watetezi wa haki za binadamu :OHCHR

wanamke akiwa anakwenda kuchota maji katika wilaya ya Chikwawa, Malawi.
Photo: OCHA/Tamara van Vliet
wanamke akiwa anakwenda kuchota maji katika wilaya ya Chikwawa, Malawi.

Malawi chunguzeni vitisho dhidi ya watetezi wa haki za binadamu :OHCHR

Haki za binadamu

Udhalilishaji pamoja na vitisho  wanavyokabiliana navyo watetezi wa amani nchini Malawi yafaa kuchunguzwa.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Geneva Uswisi na msemaji   wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya haki za binadamu OHCHR Liz Throssell.

Msemaji  huyo ameongeza kuwa  visa hivyo  dhidi ya watetezi wa haki za binadamu na wanaharakati nchini humo vimeongezeka ambapo visa  kadhaa vimeripotiwa katika wiki  chache zilizopita vikiwemo dhidi ya wanawake kabla ya uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika mwaka ujao.

Ofisi ya haki za binadamu pia  ina wasiwasi kutokana na mwelekeo unaojitokeza wa kutoa vitisho dhidi ya wabunge wanawake na pia wagombea wa viti mbalimbali.

Ofisi hiyo inatoa wito kwa  serikali nchini Malawi kuhakikisha kwamba  vitisho na hujuma dhidi ya  watetezi wa haki za binadamu vinachunguzwa kikamilifu na pia kazi muhimu za  wafanyakazi wa asasi za kiraia  zinalindwa kwa mujibu wa sheria za haki za binadamu za kimataifa.

Ofisi ya haki za binadami imesisitiza kuwa ni lazima  kuweka mazingira bora kabla ya uchaguzi mkuu  ili kila mtu aweze kutumia  kikamilifu haki ya kujieleza, kukusanyika kwa amani na haki ya kujumuika.